Bouba Diop afariki dunia
30 Novemba 2020Matangazo
Atakumbukwa sana kwa goli alilolifunga Senegal walipokuwa wakikwaana na mabingwa wa dunia wakati huo Ufaransa katika mechi ya kwanza ya Kombe la Dunia ambapo miamba hao wa Afrika waliebuka kidedea.
Alikuwa pia kwenye kile kikosi kilichopoteza fainali ya Kombe la Mataifa barani Afrika kwa mikwaju ya penalti dhidi ya Cameroon.
Vyombo vya habari nchini Senegal vinasema kiungo huyo wa zamani amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.