Baraza la Usalama lataka Iran iache kuzilenga nchi za Ghuba
12 Machi 2026
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetoa wito kwa Iran kusitisha mashambulizi dhidi ya nchi za Ghuba, kupitia azimio ambalo halikutaja mashambulizi ya Marekani au Israel dhidi ya Iran.
Azimio hilo, lililopitishwa kwa kura 13 huku nchi mbili zikijizuia, linataka kusitishwa mara moja kwa mashambulizi yote yanayofanywa na Iran dhidi ya Bahrain, Kuwait, Oman, Qatar, Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu na Jordan.
Pia linalaani hatua au vitisho vyovyote vinavyofanywa na Tehran, vinavyolenga kufunga au kuzuia safari za meli za kimataifa kupitia Mlango Bahari wa Hormuz.
Balozi wa Iran, Amir Saeid Iravani, alisema kupitishwa kwa azimio hilo ni matumizi mabaya ya wazi ya mamlaka ya Baraza la Usalama kwa ajili ya kulinda maslahi ya kisiasa ya Marekani na Israel.