1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Afisa wa zamani wa riadha Okeyo afungiwa maisha michezoni

Sekione Kitojo
31 Agosti 2018

Afisa mwandamizi wa zamani wa chama cha riadha nchini Kenya David Okeyo amepigwa marufuku maisha kushiriki katika mchezo huo  na kutozwa faini ya dola 50,000 kwa ubadhirifu wa fedha za chama hicho.

https://p.dw.com/p/343g1
David Okeyo IAAF Kongress Peking China
David Okeyo , afisa mwandamizi wa shirikisho la riadha nchini Kenya AKPicha: Getty Images/L. Zhang

David Okeyo  amepigwa  marufuku  kushiriki  katika  uongozi  wa  chama  hicho  maisha baada ya kupatikana na hatia ya kuchukua mamia kwa maelfu ya dola za malipo ya ufadhili kwa  matumizi yake binafsi.

Okeyo, katibu  mkuu  wa  zamani  na  makamu  wa  rais  wa  chama cha  Riadha  nchini  Kenya  AK, pamoja  na  kuwa  mjumbe  wa baraza  la  shirikisho  la  vyama  vya  riadha  duniani IAAF, na Joseph Kinyua, mweka  hazina  wa  zamani  wa  chama  hicho, walikuwa  wakichunguzwa  na  bodi  ya  maadili  ya  michezo kuhusiana  na  malipo yaliyofanywa  na  kampuni  ya  vifaa  vya michezo  ya  Marekani Nike kati  ya  mwaka  2003  na  2015.

UK Leichtathletik-WM: Kenianer Kirui holt Marathon-Gold
Mmoja kati ya wanariadha wa Kenya Kipkorir Kirui mjini LondonPicha: Reuters/T. Melville

Katika  hukumu  iliyomo  katika  kurasa 74 na  kutolewa  leo Alhamis, bodi  hiyo  iligundua  kwamba  katika  nyakati  kadhaa  Okeyo hakuweza  kukieleza   chama  hicho  cha  Riadha  cha  Kenya kutolewa  kwa  fedha  zilizotolewa  na  kampuni  ya  Nike  alikofanya kutoka  katika  akaunti  ya  benki  ya  chama  cha  riadha  na  pia hakuweza  kuonesha  ushahidi  wowote  juu  ya  matumizi  ya  fedha hizo.

Kwa  hiyo  amepatikana  na  hatia  ya  kukiuka  maadili   mara  10 baada  ya  kuchukua  fedha  hizo  za  ufadhili  ambazo "zingeweza kuelekezwa  katika   kusaidia  maendeleo  ya  mchezo  huo  wa riadha  nchini  Kenya" na  kuondolewa  kutoka  katika  nafasi  yake katika  baraza  la  IAAF.

Brasilien Rio 2016 800 Meter Finale der Männer David Lekuta Rudisha
wanariadha wa Kenya huvaa sare zilizotengenezwa na kampuni ya Nike ya MarekaniPicha: picture-alliance/dpa/S. Suki

Kinyua  alikutikana  na  bodi  hiyo  "kufanya  tabia  kama  hiyo" lakini hakuwa  afisa  wa  IAAF  katika  wakati  huo, ilionekana  kwamba hafungwi  na  sheria  hiyo  ya  maadili   katika  wakati  huo  na  kwa hivyo  ameepuka  adhabu.