Raia wa Msumbiji wanapiga kura hii leo kuchagua rais na wawakilishi wao watakaowaongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo. Rais Felipe Nyusi anatarajiwa kushinda awamu ya pili ya uongozi//Shirika la Human Right Watch, limetoa wito kwa serikali ya Uganda kufanya uchunguzi wa kina juu ya kifo cha mwanaharakati wa kutetea haki za watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja kilichotokea Oktoba 4