1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON:Fischer yuko Washington

17 Novemba 2003
https://p.dw.com/p/CG0G
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Yoschka Fischer amewasili mjini Washington ambapo mazungumzo yake na maafisa wa serikali ya Marekani yanatarajiwa kulenga suala la Iraq. Fischer anatazamiwa leo hii kukutana na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Colin Powell na mshauri wa usalama wa taifa Condeleeza Rice. Baadae wiki hii Fischer ataelekea New York kwa mazungumzo katika Umoja wa Mataifa.