1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Washington. Wamarekani weusi waandamana.

16 Oktoba 2005
https://p.dw.com/p/CERQ

Mamia kwa maelfu ya Wamarekani weusi wameandamana dhidi ya hali ya kutokuwa na usawa nchini humo, katika maandamano mjini Washington katika maadhimisho ya miaka 10 ya maandamano yaliyojulikana kama , maandamano ya watu milioni moja.

Mmoja kati ya waandaaji wa maandamano hayo , kiongozi wa taifa la Kiislamu nchini Marekani Louis Farrakhan , amesema kuwa serikali kuu imeshindwa kuwasaidia waathirika ambao wengi wao walikuwa Wamarekani weusi wakaazi wa New Orleans baada ya kimbunga Katrina.

Farrakhan , ameshauri kuwashitaki mawakala wa serikali kuu kwa kushindwa kutimiza wajibu wao wakati maafa hayo yanatokea, ambapo zaidi ya watu 1,000 wamepoteza maisha yao katika pwani ya Mexico.