Gavana Carly Kasivita Nzanzu amefanya ziara wilaya ya Beni, DR Kongo wakati wananchi wa eneo hilo wakiaandamana kukishinikiza kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani nchini Kongo, MONUSCO kuondoka nchini humo. Wakaazi wa Beni wanadai askari hao wanashindwa kuwalinda huku wakiendelea kuuawa na waasi wa ADF kutoka Uganda.