Wafaransa wamchagua rais kesho
21 Aprili 2007Matangazo
PARIS:
Watetezi mashuhuri kabisa katika uchaguzi wa hapo kesho wa rais nchini Ufaransa, walifanya jana kampeni yao ya mwisho kuvutia kura upande wao.Usoni kabisa ni mtetezi wa chama-tawala cha kiConservative Nocolas Sarkozy na Bibi Segolene Royal wa chama cha kisoshalist.Nafasi ya tatu anafuatia Francois Bayrou wa jukwaa la kati na Jean-Marie le Pen,mkongwe wa mrengo wa kulia kabisa.Ikiwa kama inavyotarajiwa hakuna atakeibuka na ushindi duru ya kwanza hapo kesho, duru ya pili imepangwa Mei 6.