1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroYemen

Waasi wa Houthi wakiri kushambulia meli ya Uholanzi

1 Oktoba 2025

Waasi wa Houthi nchini Yemen hii leo wamedai kuhusika na shambulizi la meli ya mizigo ya Uholanzi wiki hii katika njia inayotumiwa na idadi kubwa ya meli kwenye Ghuba ya Aden.

https://p.dw.com/p/51JFa
Bahari ya Shamu 2024 | Jaribio la kuokoa meli ya mafuta iliyokuwa ikiungua katika Bahari ya Shamu baada ya mashambulizi ya waasi wa Houthi wa Yemen, Septemba 14, 2024.
Jaribio la kuokoa meli ya mafuta iliyokuwa ikiungua katika Bahari ya Shamu baada ya mashambulizi ya waasi wa Houthi wa Yemen, Septemba 14, 2024. Picha: ropean Union's Operation Aspides/AP/picture alliance

Meli hiyo ya mizigo MV Minervagracht ilishambuliwa na kombora siku ya Jumatatu lililowajeruhi watu wawili na kusababisha moto, hii ikiwa ni kulingana na mmiliki wa meli.

Waasi hao wamesema kwenye taarifa iliyotangazwa na shirika lake la habari la Saba kwamba waliilenga meli hiyo kwa sababu kampuni inayomiliki ilikiuka uamuzi wa kupiga marufuku kuingia katika bandari za Palestina inayokaliwa kwa mabavu.

Waasi hao wanaoungwa mkono na Iran wanafanya mashambulizi ya meli za kibiashara kama ishara ya kuwaunga mkono Wapalestina katikati ya vita vya Israel na Hamas huko Gaza.