Ungana naye Fathiya Omar ambaye katika makala ya Utamaduni na Sanaa anayezungumzia namna usasa ulivyoathiri muziki wa taarabu mjini Mombasa, ambako muziki huo ni mashuhuri. Muziki huo sasa umekuwa ukipigwa na ladha za kisasa na kuondoa uasili wake ambapo taarabu ilijulikana sana kwa watu wa mwambao kuwa muziki wa kistaarabu.