1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yailaumu Ukraine juu ya makubaliano ya kusitisha vita

9 Mei 2026

Wizara ya ulinzi ya Urusi imeishtumu Ukraine kwa kukiuka makubaliano ya siku tatu ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Rais wa Marekani Donald Trump.

https://p.dw.com/p/5DWfm
Marekani  Washington D.C. 2025 | Putin na Zelensky
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky( kushoto) na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin (kulia)Picha: Mandel Ngan/Andrew Caballero-Reynolds/AFP

Likinukuu taarifa ya wizara hiyo ya ulinzi, shirika la habari la Interfax limeripoti kuwa vikosi vya Ukraine vilikuwa vimelenga maeneo ya kijeshi ya Urusi na miundombinu ya raia kwa kutumia droni na makombora.

Ripoti hiyo pia imesema mikoa ya Kaluga, Tula, Smolensk, Kursk, Bryansk na Belgorod  nchini Urusi imeshambuliwa pamoja na Jamhuri ya Chechen na mikoa ya Stavropol na Krasnodar kusini mwa Urusi.

Hakukuwa na uthibitisho wa mashambulizi hayo kutoka upande wa Ukraine, lakini maafisa wake wakuu wameripoti mashambulizi 45 ya Urusi mapema leo katika eneo la Donbass mashariki mwa  Ukraine.

Wizara ya ulinzi ya Urusi pia imeripoti mashambulizi 12 ya Ukraine. Hata hivyo taarifa za pande hizo mbili hazikuweza kuthibitishwa kwa njia huru.