1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Urusi yaendelea kuishambulia Ukraine kwa droni

13 Februari 2026

Watu sita wameuawa katika mashambulizi yaliyofanywa na Urusi kote nchini Ukraine usiku wa kuamkia leo, na hususan yakilenga mji wa pwani wa Odesa na miundombinu ya nishati, hii ikiwa ni kulingana na maafisa.

https://p.dw.com/p/58fpA
Ukraine Odessa 2026 | Uharibifu baada ya shambulio la Urusi kwenye makazi na soko
Urusi imeendelea kuishambulia Ukraine na hasa miundombinu yake ya kusambaza joto na kusababisha hali tete kwa raia wa nchi hiyo.Picha: Oleksandr Gimanov/AFP

Urusi ilifyatua droni 154, limesema jeshi la anga la Ukraine na kuonya kuwa droni nyingine bado zingali kwenye anga la Ukraine.

Watu watatu na mvulana mmoja waliuliwa usiku wa jana katika jiji la Kramatorsk, zimesema mamlaka za eneo hilo.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky kwenye hotuba yake ya jana jioni, alizitolea wito nchi washirika barani Ulaya kuharakisha utoaji wa mifumo ya ulinzi wa anga, akisema mashambulizi mapya ya makombora na droni kutoka Urusi yanaendelea kuhatarisha maisha ya raia na miundombinu muhimu nchini humo.