MigogoroUkraine
Ukraine yahofia mbinu mpya za mashambulizi ya Urusi
13 Mei 2026
Matangazo
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema mamia ya droni yalikuwa kwenye anga ya Ukraine wakati Moscow ikiwa imebadilisha mbinu na kushambulia zaidi nyakati za mchana.
Tangu vita hivyo vilipoanza miaka minne iliyopita Urusi imekuwa ikifanya mashambulizi makubwa majira ya usiku, lakini katika wiki za karibuni imefanya mashambulizi kama hayo mchana na kuvuruga pakubwa shughuli za wakaazi.
Hata hivyo, Urusi imekanusha kuwalenga kwa makusudi raia lakini tayari imewaua maelfu wakati wa vita, na kwa upande mwingine ikijipa uhalali wa kushambulia miundombinu ya raia, kama mbinu ya kudhoofisha uwezo wa Ukraine vitani.