Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres azikosoa nchi zilopuuza mwongozo wa awali wa WHO kuhusu virusi vya corona. Umoja wa Mataifa umesema utapiamlo waongezeka Yemen na janga la njaa haliwezi tena kuepukika. Na, Israel yawaonya raia wake walio nje ya nchi kuwa na tahadhari dhidi matamshi ya vitisho ya Iran.