1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shambulizi la Urusi nchini Ukraine lawajeruhi watu 11

31 Oktoba 2025

Urusi imefanya mashambulizi ya usiku kucha katika mji wa Sumy kaskazini mashariki mwa Ukraine na kuwajeruhi wakazi 11 ikiwemo watoto wanne. Hayo yamesemwa leo na huduma za dharura za Ukraine.

https://p.dw.com/p/52sMH
Ukraine Sumy 2025 | Shambulizi la droni
Shambulizi la Urusi katika mji ya Sumy nchini UkrainePicha: State Emergency Service of Ukraine/REUTERS

Kupitia ujumbe uliochapishwa kwenye  mtandao wa Telegraph, kitengo hicho cha huduma za dharura kimesema shambulizi hilo la Urusi lililenga jengo la makazi la ghorofa, nyumba binafsi pamoja na miundombinu.

Gavana wa eneo hilo Ihor Kalchenko, amesema Urusi ilikuwa imeshambulia pia karakana ya reli na kuharibu mabehewa kadhaa na majengo.

Eneo hilo la Sumy linapakana na Urusi na limekuwa chini ya mashambulizi ya mara kwa mara ya droni na makombora.