1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Imani

Papa Leo akosoa ukosefu wa usawa barani Afrika

22 Aprili 2026

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo XIV amewatolea wito watu wa Guinea ya Ikweta kufanya kazi kwa ajili ya uhuru, haki na kupunguza pengo kati ya walionacho na maskini.

https://p.dw.com/p/5CfVh
Mapokezi ya Papa, Malabo, Guinea ya Ikweta
Papa Leo XIV akipokelewa baada ya kuwasili Malabo, Guinea ya Ikweta, pembeni yake ni Rais Teodoro Obiang Nguema MbasogoPicha: Alberto Pizzoli/AFP

 Ameyasema hayo katika Misa Takatifu aliyoiongoza mjini Mongomo ambapo amezungumzia pia ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo na kuwaombea heri watu wa nchi hiyo.

Waafrika waaswa kulinda heshima na utu

Katika misa hiyo amenukuliwa akisema kuwa, "Nawaombea uhuru uongezeka na heshima ya mtu ilindwe siku zote. Ninawafikiria masikini na familia zinazopitia magumu. Ninawakumbuka wafungwa ambao mara nyingi wanalazimika kuishi kwenye mazingira magumu ya usafi na afya."

Baada ya misa hiyo Papa Leo alielekea kulitembelea gereza maarufu katika mji wa Bata ili kuwapa matumaini wafungwa na kuwakumbusha kuwa kanisa liko pamoja nao.