Algeria ni miongoni mwa mwa mataifa yaliyo katika mzozo mkali wa kisiasa. Kwa wiki kadhaa imegubikwa na maandamano, raia wakidai mabadiliko ya haraka. Rais Abdelaziz Bouteflika naye akachochea makali baada ya kutangaza nia yake ya kugombea muhula wa tano. Mengi kuhusu mzozo huo yanajadiliwa hapa kwenye Maoni mbele ya Meza ya duara.