Meunier alenga kupata mataji akiwa na Dortmund
16 Julai 2020"Iwapo utaangalia ubora wa kikosi, katika miaka ijayo klabu ni lazima ishinde kitu tena," mchezaji huyo wa ulinzi kutoka Ubelgiji aliliambia shirika la habari la Ujerumani dpa.
"Na tutafanya hivyo. Mapenzi yangu kwa ushindi na mataji hayana ukomo."
Meunier , mwenye umri wa miaka 28, ameshinda ligi ya Ubelgiji na kikombe cha chama cha mpira akiwa na Club Brugge na alipata mataji matatu mfululizo akiwa katika Ligue 1 nchini Ufaransa pamoja na vikombe kadhaa akiwa na PSG. Mlinzi huyo wa kulia alikuwa sehemu ya kikosi cha Ubelgiji ambacho kilimaliza katika nafasi ya tatu katika kombe la dunia mwaka 2018.
Meunier angependa kuchelewesha kuwasili kwake Dortmund kwa wiki chache kuweza kushuhudia taji moja zaidi akiwa na PSG lakini makubaliano kumuwezesha yeye kucheza katika michuano ya fainali ya Champions League mwezi Agosti mjini Lisbon hayakuweza kufikiwa.
Meunier alitaka kubakia kwa muda PSG
Maafisa wa Dortmund walikuwa tayari, Meunier alisema, lakini mkurugenzi wa spoti wa PSG Leonardo hakuwa tayari kwa hilo.
"Leonardo hakuwa katika wakati wowote akitaka kutafuta makubaliano na Dortmund, licha ya mimi," Meunier alisema. "Alitaka mimi kuitumikia PSG bure."
Badala yake alifahamishwa kupitia barua ya wakili kukaa mbali na viwanja vya klabu hiyo. wakili wake alijaribu kumpatia yeye nafasi kwa ajili ya kufanya mazowezi, kutokana na vizuwizi vya virusi vya corona, lakini jaribio hilo lilikataliwa.
"Kisha nikaambiwa kwa simu kuwa nisijaribu kuvuka mstari wa yeyote yule kwasababu naweza kusimulia hadithi za kukera hapo baadaye," Meunier alisema. "Ni hali ya kukosa uhalisia."
"Leonardo aliwaambia waandishi habari nchini France kuwa nimekataa kurefushwa mkataba. Lakini hiyo si sahihi, natak kusema hilo wazi."
Meunier anakosoa pia uamuzi wa Ufaransa na Ubelgiji kufuta msimu uliopita wa ligi kwasababu ya virusi vya corona na sio kuanzisha tena kama ilivyokuwa kwa ligi zingine kubwa barani Ulaya.