Mawaziri wa mambo ya nje wa BRICS wakutana nchini India
14 Mei 2026
Mkutano huo unawaleta pamoja wanadiplomasia kutoka Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini pamoja na nchi wanachama wapya.
Katika mkutano huo, waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araghchi aliyahimiza mataifa ya BRICS kuzilaani Marekani na Israel kwa kile alichokiita "uchokozi wao usio halali" dhidi ya Tehran.
"Tuko tayari kupigana kwa kutumia kila kitu tulichonacho kwa ajili ya kutetea uhuru wetu na ardhi yetu, lakini pia tuko tayari kufuata na kusimamia diplomasia. Kama ambavyo nimekuwa nikisema wakati wote halitapatikana suluhisho la kijeshi katika kutatua chochote kinachohusiana Iran.
Araghchi amesema ni muhimu kwa wote kuongeza juhudi za kukomesha hali ya ubora na kutokujali kwa upande wa Marekani, dhana aliyosema haina nafasi katika ulimwengu wa leo.