MALIBU:wakimbia moto Carlifornia
23 Oktoba 2007Matangazo
Maalfu ya watu wamekimbia nyumba zao kutokana na mioto mikubwa ambayo hadi sasa inashindikana kudhibitiwa katika Carlifornia.
Habari zinasema mioto mikubwa 13 inaendelea kuwaka kusini mwa Carlifornia na mtu mmoja amekufa na wengine 20 wamejeruhiwa.
Mioto hiyo imesababishwa na kipindi kirefu cha ukosefu wa mvua.