Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani WHO, takriban watu bilioni moja duniani kote wanaugua magonjwa ambayo hayapewi kipaumbele, huku watu bilioni mbili wakiwa katika hatari ya kuyapata magonjwa hayo. Katika Makala ya Afya Yako, leo tunaangazia magonjwa ya matende na mabusha ambayo ni miongoni mwa magonjwa yasiyopewa kipaumbele katika jamii. Mtayarishaji na msimulizi ni Salma Mkalibala.