Je, twaweza kuitenganisha lugha na utamaduni wa wenye lugha yenyewe? Je, ili mtu kuitwa Mswahili ni lazima awe mwenye utamaduni wa Kiswahili? Ndiyo maswali ambayo Mohammed Khelef anajadiliana na Dk. Ahmad Pakar kutoka nchini Kenya, akitaka kujuwa endapo panaweza kuwapo Kiswahili bila ya kuwapo Waswahili na au kinyume chake.