Israel yaharibu kamera 17 za uangalizi za UN nchini Lebanon
4 Aprili 2026
Afisa mmoja wa uslama aliyezungumza na shirika la habari la AFP kwa sharti la kutotajwa jina, amesema kamera hizo ziliharibiwa na jeshi la Israel katika mji wa pwani wa Naqura.
Hapo jana UNIFIL iliripoti kutokea kwa mlipuko katika moja ya kambi zake karibu na Odaisseh kusini mwa Lebanon na kujeruhiwa kwa maafisa wake watatu.
Hata hivyo imesema bado hawajafahamu ulipotokea mlipuko huo.
Kwa upande wake, jeshi la Israel limelishtumu kundi la Hezbollah kwa kurusha roketi iliyoanguka kwenye jengo la UNIFIL .
Ofisi ya Umoja wa Mataifa huko Jakarta imesema leo kuwa waliojeruhiwa ni raia wa Indonesia.
Indonesia imeshtumu tukio hilo na kulitaja kuwa lisilokubalika na kuongeza kuwa matukio hayo yanasisitiza haja ya dharura ya kuimarisha ulinzi kwa vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa.