JamiiIsrael
Israel: Uingereza idhibiti chuki dhidi ya Wayahudi
29 Aprili 2026
Matangazo
Kupitia mtandao wa X, wizara hiyo imeikosoa serikali ya Uingereza kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo ikiangazia kuanzia mashambulizi kwenye masinagogi, taasisi za Kiyahudi, magari ya wagonjwa ya jamii hiyo hadi kisa hiki cha sasa.
Wizara hiyo imesisitiza kwamba maneno tu hayatoshi kukabiliana na mizizi ya chuki dhidi ya Wayahudi inayoenea kote Uingereza na kuitaka serikali ya Waziri Mkuu Keir Starmer kuchukua hatua na maamuzi ya haraka.
Rais wa Israel Isaac Herzog kwa upande wake amesema ameshtushwa na shambulizi hilo na kusema wakati umefika sasa kwa ulimwengu kuanza kupambana na wimbi hili la kutisha la chuki dhidi ya Wayahudi kwa namna yoyote ile.