Iran yashambulia Israel na mataifa jirani ya Ghuba
18 Machi 2026
Matangazo
Mashambulizi mapya yaliripotiwa mapema leo, katika mkoa mkubwa wa mashariki wa Saudi Arabia, ambao ni makazi ya visima vyake vingi vya mafuta, Kuwait, Bahrain, Qatar na Umoja wa Falme za Kiarabu.
Nchini Iran, kinu cha nyuklia cha Bushehr kililengwa kwa kombora lakini hakukuwa na majeraha wala uharibifu. Haya ni kulingana na Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki IAEA baada ya kupokea ripoti kutoka Tehran.
Mkuu wa IAEA, Rafael Grossi, amesisitiza wito wake wa kujizuia zaidi wakati wa mzozo huo ili kuzuia hatari ya ajali ya nyuklia.