1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Vifo na majeruhi wa Urusi na Ukraine huenda wakafika mil.2

29 Januari 2026

Idadi ya wanajeshi wa Urusi na Ukraine waliokufa, kujeruhiwa ama kupotea huenda ikafikia milioni 2 katika majira ya machipuko huku Urusi ikiwa imeathirika zaidi tangu Vita vya Pili vya Dunia.

https://p.dw.com/p/57eO3
Ukraine Zaporizhzhia 2026 | Wanajeshi wa Ukrein wanaandaa mfumo wa kupambana na vifaru wakati wa mazoezi
Wanajeshi wa Ukraine wakiandaa mfumo wa kushambulia vifaru katika mazoezi ya kijeshi kwenye mstari wa mbele katikati ya vita vikali ya Urusi huko Zaporizhzhia, Ukraine, Jan. 4, 2026. Picha: Andriy Andriyenko/Ukraine's 65th Mechanized Brigade/AP Photo/picture alliance

Ripoti ya Kituo cha Masomo ya Kimkakati na Kimataifa, CSIS iliyochapishwa siku ya Jumanne imesema watu milioni 1.2 wa Urusi walikufa ama kujeruhiwa, ikiwa ni pamoja na wanajeshi 325,000 waliokufa katika kipindi cha kati ya Februari 2022 na disemba 2025.

Ripoti hiyo inakadiria kwamba watu 500,000 hadi 600,000 walikufa ama kujeruhiwa nchini Ukraine ambako kuna raia na wanajeshi wachache, miongoni mwao waliokufa ni 140,000.

Takwimu hizo zinachapishwa chini ya mwezi mmoja wa maadhimisho ya miaka minne tangu Urusi ilipoivamia kikamilifu Ukraine Februari, 2024.