Uhuru wa kujieleza ni hali ya mtu kutoa maoni yake juu ya kile anachokiamini. Anaweza kutoa maoni kwa njia yoyote ile. Kwa kutamka, kuandika au kwa njia ya sanaa, ilimradi uhuru huo usiwe na madhara kwa watu wengine. Katika makala ya Mbiu ya Mnyonge tunaangazia uhuru wa kujieleza na kutoa maoni nchini Tanzania.