BAGHDAD: Waingereza 5 wametekwa nyara Iraq
29 Mei 2007Matangazo
Wizara ya mambo ya nje ya Uingereza imethibitisha kuwa Waingereza 5 wametekwa nyara nchini Irak. Inasemekana watu hao walikamatwa nje ya Wizara ya Fedha ya Irak.Hapo awali maafisa wa usalama wa Iraq walisema,Wajerumani 3 pia walitekwa nyara. Lakini hadi hivi sasa,ripoti hiyo haijathibitishwa na serikali ya Ujerumani.