Kiongozi wa kundi la magaidi linalojiita "Dola la Kiislam"-IS, Abu Bakar al baghdad ameuwawa na rais wa Marekani Donald Trump anajifakharisha kwa "ufanisi" walioupata// Rais wa Baraza Kuu la Ulaya Donald Tusk amesema viongozi wa nchi ishirini na saba za Umoja wa Ulaya watakubali kuongezwa kwa muda wa Uingereza kujiondoa kutoka kwenye Muungano wa Ulaya, Brexit, hadi Januari 31.