Hatua ya mahakama ya jeshi Uganda kumwondolea mashtaka ya kukutikana na bunduki mbunge na msanii maarufu Bobi Wine imepokelewa kwa shangwe na wafuasi wake, wakiamini kwamba hata kesi ya uhaini aliofunguliwa katika mahakama ya kiraia muda mfupi baada ya kuachiliwa itatupiliwa mbali kwa mtazamo kuwa inachochewa na tofauti za kisiasa kati yake na utawala wa rais Museveni.