Yanayojiri ulimwenguni kote juu ya janga la ugonjwa wa virusi vya corona Covid-19: wafanyibiashara Kenya walalamikia hasara kubwa kutokana na marufuku masoko ya wazi. Taasisi ya saratani ya Ocean road nchini Tanzania imepunguza kiwango cha ndugu ambao wanaoruhusiwa kumuona mgonjwa, Ikiwa ni sehemu ya hatua za kudhibiti kuenea kwa maambukizi ya virusi vya Corona.