Hii leo, marais wa Kenya na Uganda wameshuhudia kusainiwa kwa mkataba wa amani kati ya jamii za wafugaji za Karamoja, Turkana na Pokot// Baraza la Viongozi wa kidini Barani Afrika limewataka viongozi wa Afrika Mashariki kuwashinikiza Rais Salva Kiir na kiongozi wa upinzani nchini Sudan Kusini Riek Machar kutekeleza mkataba wa amani kwa nia njema.