Leo imetimia miaka kumi tangu maandamano ya msimu wa machipuko ya mwaka 2011 nchini Yemen// Marekani, Wademocrat wanaendelea leo kuwasilisha hoja zao katika kesi dhidi ya rais wa zamani Donald Trump ambayo inasikilizwa kwenye Baraza la Seneti mjini Washington// Rais wa Marekani Joe Biden na Xi Jinping wamefanya mazungumzo yaliyojikita juu ya ukiukaji wa haki za binadamu katika eneo la Xinjiang.