Muungano wa unaoongozwa na Saudi Arabia katika vita nchini Yemen umetetea shambulio la angani lililotokea katika eneo la Kaskazini mwa nchi hiyo ambalo lilisababisha vifo vya watu arubaini na tatu. Waasi wa kabila la Houthi wamesema kwamba shambulio hilo lililenga basi ambalo lilikuwa limewabeba wanafunzi walio chini ya umri wa miaka kumi na mitano.