Serikali ya Yemen inayoungwa mkono na saudi Arabia na waasi wa kusini wanaotaka kujitenga wametia saini makubaliano jana kumaliza mvutano wa kuwania madaraka katika eneo la kusini ya Yemen// Chama cha Democratic kimeibuka na ushindi katika uchaguzi wa gavana katika jimbo la Kentucky// DR Congo- ADF waliwauwa watu kumi katika mji mdogo wa Kokola ulio kilomita arubaini kaskazini mwa mji wa Beni.