Idadi jumla ya watu waliokufa kutokana na virusi vya Corona duniani imefikia zaidi ya robo milioni hii leo Jumanne// Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania Chadema kinaonekana kugawika baada ya wabunge wake kadhaa kukaidi agizo la chama hicho kususia vikao vya bunge// Congo ni nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili ulimwenguni baada ya Syria kwa idadi kubwa ya wakimbizi wa ndani.