Viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya waliopo katika mkutano wa kilele nchini Malta, wanatafuta msimamo wa pamoja dhidi ya Rais wa Marekani, Donald Trump// Wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo wakiendelea na maombolezo ya kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini humo na mwanasiasa mkongwe Etienne Tshisekedi, kunatarajiwa kuwepo na mtikisiko kwa upande wa upinzani.