1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 55 wameuwawa mashariki mwa DRC

1 Juni 2021

Umoja wa Mataifa umesema watu wapatao 55 wameuwawa usiku wa kuamkia leo katika mashambulizi mawili yaliyofanywa kwenye vijiji mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

https://p.dw.com/p/3uGu3
Demokratische Republik Kongo Soldaten Patroullie nahe Beni
Picha: picture-alliance/AP Images/Al-Hadji Kudra Maliro

Umoja wa Mataifa umesema watu wapatao 55 wameuwawa usiku wa kuamkia leo katika mashambulizi mawili yaliyofanywa kwenye vijiji mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mashambulizi hayo yanaelezwa kuwa machafuko mabaya ya usiku kuwahi kushuhudiwa katika eneo hilo katika takriban miaka minne.

Jeshi pamoja na mashirika ya kutetea haki za kiraia katika eneo hilo yamelinyooshea kidole cha lawama kundi la waasi la Allied Democratic Forces, ADF kwa kukivamia kijiji cha Tchabi na kambi ya watu waliolazimika kuyakimbia makaazi yao karibu na kijiji kingine cha Boga. Vijiji vyote vipo karibu na mpaka wa Uganda.

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya kibinaadam limesema katika taarifa yake kwamba nyumba ziliteketezwa kwa moto na raia walitekwa.