Msikilizaji Makala Yetu Leo itaangazia Azimio la Malabo la mwaka 2014, ambalo linazihimiza nchi za Afrika kutenga asilimia 10 ya bajeti zake kwa ajili ya kilimo. Makala hii leo inajikita nchini Tanzania miongoni mwa nchi zilizosaini makubaliano hayo kwa lengo la kukuza sekta ya kilimo katika taifa hilo la Afrika Mashariki. Karibu, umsikilize Veronica Natalis.