SiasaBurkina Faso
Utawala wa kijeshi wa Burkinabe wavunja vyama vya siasa
30 Januari 2026
Matangazo
Waziri wa Mamlaka za Maeneo Emile Zerbo amesema hatua hiyo imechukuliwa baada ya mamlaka kugundua kwamba vyama hivyo vinakiuka miongozo ya kuanzishwa kwao, kusababisha migawanyiko miongoni mwa wananchi na kudhoofisha muundo wa kijamii.
Shughuli za vyama vya siasa kwa muda mrefu zimezuiwa chini ya utawala wa kijeshi na amri hiyo inataka mali za vyama hivyo kuhamishiwa serikalini, limearifu shirika la habari la serikali.
Wanaharakati wanasema hatua kama hizo zimelenga uhuru wa raia na upinzani tangu mamlaka ya kijeshi ilipochukua mamlaka katika mapinduzi ya 2022.