Hamburg inajulikana sana kwa shughuli za majini kutokana na uwepo wa bandari, mto elbe, na ziwa Alster.Ziwa Alster ni kitovu cha maisha ya mji wa Hamburg. Limegawanyika katika maeneo mawili yani Alster ya ndani na ile ya nje ambayo hutiririsha maji yake katika mto Elbe kusini mwa mji unaoiunga Hamburg na bahari ya kaskazini.