1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBrazil

Ujerumani yaahidi kusaidia ulinzi wa msitu wa Amazon

Iddi Ssessanga
31 Januari 2023

Ujerumani imeahidi kutoa msaada wa Euro milioni 200 kuisaidia Brazil kuulinda msitu wa mvua wa Amazon.

https://p.dw.com/p/4MuM2
Brasilien | Luiz Inacio Lula da Silva trifft Olaf Scholz
Picha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Ujerumani imeahidi kutoa msaada wa Euro milioni 200 kuisaidia Brazil kuulinda msitu wa mvua wa Amazon. Tangazo hilo limetolewa wakati wa ziara ya Kansela Olaf Scholz mjini Brasilia. Scholz ambaye anaizuru Brazil baada ya kuzitembelea Chile na Argentina, amesema amefurahishwa na kurejea kwa Brazil katika jukwaa la dunia. Msaada huo unajumuisha mfuko mpya wa euro milioni 31 kwa ajili ya majimbo ya Brazil kusaidia ulinzi wa msitu huo, na euro milioni 93 zitaelekezwa kwenye miradi ya upandaji tena miti. Kansela wa Ujerumani amesema Berlin inataka maendeleo ya haraka katika makubaliano ya biashara huria kati ya Umoja wa Ulaya na jumuiya ya Mercosur.