Kuwa na tatizo la kutopata choo maana yake ni kwamba unapata choo kigumu ama unapata kwa shida. Muda wa kupata haja kubwa hutofautiana kati ya mtu na mtu. Lakini unapokosa choo kwa siku tatu na zaidi, huwa ni muda mrefu. Katika Afya Yako utaelezwa kinachosababisha kukosa choo na cha kufanya kuondokana na shida hiyo.