Mwandishi mashuhuri wa kazi za fasihi kutoka Kenya, Ngugi wa Thiong’o, yupo nchini Ujerumani akihudhuria uzinduzi wa tafsiri ya Kijerumani ya kitabu chake kiitwacho Decolonizing the Mind, yaani "Kuikomboa Akili". Kwa mtazamo wake, mtu anayejua lugha nyingi bila kuijua lugha ya mama ni mtumwa wa akili. Msikilize katika kipindi cha Kinagaubaga.