1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Myanmar yahusishwa na mauwaji

Admin.WagnerD22 Aprili 2013

Shiriki la kutetea Haki za binaadamu la Human Rights Watch limetuhumu serikali ya Myanmar kwa kuendesha kampeni ya mauwaji ya kikabila ya dhidi ya kabila la dogo la waislamu la Rohingya.

https://p.dw.com/p/18KXB
Ethnic Rohingya refugees from Myanmar wave as they are transported by a wooden boat to a temporary shelter in Krueng Raya in Aceh Besar April 8, 2013. About 74 Rohingya refugees, who were heading for Australia, were found stranded on Aceh island by Indonesian fishermen on Sunday, a police official said on Monday. REUTERS/Junaidi Hanafiah (INDONESIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST TPX IMAGES OF THE DAY)
Wakimbizi wa RohingyaPicha: Reuters

Shirika hilo limetoa tuhuma hizo kwa kuzingatia ushahidi wa makabuli ya halaki na kuwepo kwa idadi kubwa ya watu waliopoteza makaazi yao.

Kwa mujibu wa ripoti ya shirika hilo lenye makao yake New York nchini Marekani, kabila la Rohingya, ambao wanadai kuwa ni raia wa taifa hilo ambalo vilevile linajulikana kama Burma, wanakabiliwa na vitendo vya kihalifu dhidi ya binaadamu yakiwemo mauwaji, mateso,kufukuzwa na kulazimika kuhama makazi yao.

Makundi ya wahusika wa tuhuma

Human Rights Watch limewataja maafisa wa Myanmar, viongozi kwa umma na viongozi wa madhehebu ya Budha kwamba wanapanga na kuvishawishi vikundi mbalimbali ambavyo vinaungwa mkono na vikosi vya usalama kufanya mashambulio ya kupanga katika vijiji vya waislamu mwezi Oktoba, huko katika jimbo la magharibi la Rakhine nchini humo.

A woman stands behind a police line near a mosque and school dormitory that were damaged by a fire in Yangon April 2, 2013. An electrical fire at an Islamic school in Myanmar's biggest city killed 13 children early on Tuesday, authorities said. The children, all boys, died of suffocation in the fire at the dormitory of a school next to the mosque in Yangon at about 2:40 a.m., neighbours and officials said. REUTERS/Soe Zeya Tun (MYANMAR - Tags: DISASTER RELIGION EDUCATION)
Mwanamke amesimama mbele ya polisiPicha: Reuters

Phil Robertson ambae ni naibu mkurugenzi wa shirika hilo katika kanda ya Asia alisisitiza kufanywa kwa vitendo hivyo kwa kudai serikali ya Myanmar inajihusisha vitendo hivyo vya ukandamizaji ambavyo vinaendelea mpaka sasa kwa kushindwa kulitambua kundi hilo la watu na kuwazuwia wasitembee kutoka sehemu moja kwena nyingine.

Hatma ya vikwazo wa Myanmar

Ripoti hii ya Human Right Watch inatolewa siku moja sambamba na siku ambayo Umoja wa Ulaya unatarajiwa kuondowa vikwazo vyake vyote vilivyosalia isipokuwa vya silaha. Kutokana na hayo Robertson anasema ni hatua ya mapema na iliyokosa maana na kwamba itashusha hadhi ya uhusiano wa Umoja Ulaya na utawala wa nchi hiyo

Burmese soldiers clearing the streets during a crackdown on pro democracy demonstrators in 1988, Rangoon, Myanmar.
Jeshi likidhibiti waandamanaji nchini MyanmarPicha: ullstein bild-Heritage Images/Alain Evrard

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Bangkok, kiongozi huyo wa Human Rights Watch ametoa wito kwa nchi wahisani zikiwemo Marekani kushinikiza Myanmar kuhamasisha mabadiliko ya kidemokrasia katika taifa hilo ambalo lilifikisha kikomo miongo kadhaa ya utawala wa kijeshi mwaka 2011.

Akielezea hali ilivyo katika jimbo la Rakhine, Robertson alionya kama hali itaendelea kama ilivyo sasa katika eneo hilo basi uenda ikazorotesha mchakato wa mabadiliko ya kidemokrasia nchini humo.

Serikali yapuuza ripoti ya HRW

Lakini msemaji wa rais wa Myanmar alilituhuma shirika la hilo kwa kutoa hadharaini ripoti yao wakati huu ambapo Umoja wa Ulaya ukitarajiwa kutoa uamuzi kuhusu vikwazo ilivyowekewa taifa hilo. Katika maelezo yake aliyoyachapisha katika ukurasa wa face book afisa huyo wa Ikulu amesema serikali itaipuuzilia mbali ripoti hiyo ya upande mmoja.

Alisema serikali inasuburi matokeo ya ripoti ya kamisheni ya timu ya maafisa wake ambao wanafanya uchunguzi ambayo hata hivyo ripoti hiyo imekuwa ikiahirishwa mara kadhaa kutolewa.

Ripoti hii ya Human Rights Watch inasema zaidi ya watu 125,000 wa Kabila la Rohingya na makundi mengine ya kiislamu wamelazimishwa kubaki pasipo makazi na kwamba wanakosa misaada ya kiutu na pia kushindwa kurejea katika makazi yao. Takwimu za serikali zinasema takribani watu 211 waliwawa katika awamu mbili tofauti za mapigano 2012 ingawa wachambuzi wanasema idadi inaweza kuwa kubwa zaidi

Mwandishi: Sudi Mnette
Mhariri:Mohammed Abdul-Rahman