Shirika lisilo la kiserikali nchini Tanzania, TWAWEZA, limeshachapisha matokeo ya utafiti yanayompa nafasi ya juu mgombea urais wa CCM, John Magufuli, dhidi ya Edward Lowassa wa UKAWA. Lakini ni kwa kiasi gani matokeo hayo yanaakisi uhalisia hivi sasa ambapo kampeni za uchaguzi zimepamba moto? Mohammed Khelef amezungumza na mwandishi wa habari muelekezi wa ripoti za uchaguzi, Attilio Tagalile.