Miaka nenda miaka rudi binaadamu amekuwa chanzo cha uharibifu wa mazingira kwa upande mwengine mara kadhaa ameweza kurejesha mazingira katika hali ya ustahamilivu. Makala ya mtu na mazingira leo hii inaangazia juhudi ambazo zimekuwa zikichukuliwa na serikali ya mji mkuu wa Rwanda, Kigali, kujaribu kuwahamisha wakaazi wa maeneo ya mabonde na kuwajengea makaazi bora na salama.