Magwiji wateremka dimbani
8 Julai 2019Matangazo
Nyota hao wanashiriki wiki ya pili ya mashindano ya Wimbledon huko Uingereza.
Mechi zote kumi na sita zimepangiwa kuchezwa Jumatatu baada ya mapumziko Jumapili.
Gauff atakuwa anapambana na mchezaji nambari moja wa zamani Simona Halep huku Serena Williams akitafuta kufuzu raundi inayofuata kwa kuchuana na Carla Suarez Navarro.
Djokovic, Nadal na Federer wote wanacheza na wachezaji ambao hawajawahi kushiriki Wimbledon.