Suala la kufanikiwa ndilo hitaji la kwanza na la msingi kwa kila binadamu mwenye akili timamu. Kila mmoja ana ndoto ambayo anatamani kuifanikisha kwa kuwa mtu fulani kwenye jamii, kupata kitu fulani ama kufika sehemu fulani anayohitaji. Hakuna mtu ambaye ana ndoto ndogo bali kila mmoja wetu anahitaji kufanikisha mipango mikubwa katika maisha yake. Je kipi kinaashiria mafanikio maishani?