Watu karibu milioni 466 duniani kote wana matatizo ya kutosikia na milioni 34 kati yake ni watoto. Inakadiriwa kuwa hadi kufikia mwaka 2050 idadi hiyo itafikia watu milioni 900 au ikimanisha kwamba mtu mmoja kati ya kumi atapoteza uwezo wa kusikia. Karibu katika makala ya Afya yako na hii leo tunalitazama tatizo la ukiziwi na kupoteza uwezo wa kusikia. Mimi ni Sylvia Mwehozi.